06 May, 2011

Siwezi simama bila Yesu!!!

Ufikapo wakati ambapo mtu huzama

Maisha hukulemea

Kilio ndicho chako kila wakati

Alfajiri na jioni wamsaka Mola

Akuinue,

Angalau akukumbuke

Maadui wamekuzingira

Hakuna cha kukuridhisha, cha kukutuliza roho

Kama Ayubu alipoteseka duniani na alimcha Mungu wakati wote

Hatujajaribiwa mpaka tukapatana na kifo

Nitamkimbilia Bwana

Yeye ndiye penzi langu

Maadui wanaposherehekea vita vyangu

Sitamsuta Maulana

Nanyenyekea mbele zake

Nikosapo nguvu

Niangukapo

Nilemewapo

Nikishushwa moyo na dunia

Napata matumaini Calvary

Alisulubiwa juu yangu

Alinifia

Akafufuka

Ili nami nipate uhai na uhai halisi

siwezi simama kwa upweke

Yesu ananishikilia kila wakati

Ata wakati huu ambapo ndugu yangu anaugua

Yesu ni Bwana

Wakati marafiki hawapatikani

Yesu yupo

Pesa haipo

Yesu yupo

Usaliti wa wapenzi

Yesu yupo

Nipo,ju Yesu yu hai ndani yangu

Siwezi simama wima pekee yangu

Lakini, nasimama juu yake Yesu!!!!

No comments:

Post a Comment

Share this, put a smile on someone's face :-)